Kut. 30:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Nawe fanya madhabahu ya kufukizia uvumba; utaifanyiza kwa mti wa mshita.

2. Urefu wake utakuwa dhiraa moja, na upana wake dhiraa moja; itakuwa mraba; na kwenda juu kwake dhiraa mbili; pembe zake zitakuwa za kitu kimoja nayo.

3. Nawe utaifunikiza dhahabu safi juu yake, na mbavu zake kando kando, na pembe zake; nawe utaifanyia ukingo wa dhahabu kuizunguka.

4. Kisha utaifanyia pete mbili za dhahabu, chini ya ukingo wake katika mbavu zake mbili, katika pande zake mbili utazifanya; nazo zitakuwa mahali pa kuitia miti ya kuichukulia.

5. Na ile miti utaifanya kwa mti wa mshita, na kuifunikiza dhahabu safi.

Kut. 30