6. Nawe fanya miti kwa ajili ya madhabahu, miti ya mshita, na kuifunika shaba.
7. Na hiyo miti itatiwa katika pete, na ile miti itakuwa katika pande mbili za madhabahu, wakati wa kuichukua.
8. Uifanye ya mbao, yenye mvungu ndani yake; kama ulivyoonyeshwa mlimani, ndivyo watakavyoifanya.