35. na tovu chini ya matawi mawili la kitu kimoja nacho, na tovu chini ya matawi mawili la kitu kimoja nacho, na tovu chini ya matawi mawili la kitu kimoja nacho, kwa hayo matawi sita yatokayo katika kile kinara.
36. Matovu yake na matawi yake yatakuwa ya kitu kimoja nacho; kiwe chote pia kazi moja ya kufua, ya dhahabu safi.
37. Nawe zifanye taa zake saba; nao wataziwasha hizo taa zake, zitoe nuru mbele yake.
38. Na makoleo yake, na visahani vyake, vyote vitakuwa vya dhahabu safi.
39. Kitafanywa cha talanta moja ya dhahabu safi, pamoja na vyombo hivi vyote.
40. Nawe angalia ya kwamba uvifanye kama mfano wake, ulioonyeshwa mlimani.