13. Yoshua akawaangamiza Amaleki na watu wake kwa ukali wa upanga.
14. BWANA akamwambia Musa, Andika habari hii katika kitabu iwe ukumbusho, kisha ihubiri masikioni mwa Yoshua; ya kuwa nitaufuta ukumbusho wa Amaleki kabisa, usiwe tena chini ya mbingu.
15. Musa akajenga madhabahu, akaiita jina lake Yehova-nisi;
16. akasema, BWANA ameapa; BWANA atakuwa na vita na Amaleki kizazi baada ya kizazi.