Kut. 16:24-28 Swahili Union Version (SUV)

24. Basi wakakiweka hata asubuhi, kama Musa alivyowaagiza; nacho hakikutoa uvundo wala kuingia mabuu.

25. Musa akasema, Haya, kuleni hiki leo; kwa kuwa leo ni Sabato ya BWANA; leo hamtakiona nje barani.

26. Siku sita mtaokota; lakini siku ya saba ni Sabato, siku hiyo hakitapatikana.

27. Ikawa siku ya saba wengine wakatoka kwenda kukiokota, wasikione.

28. BWANA akamwambia Musa, Mtakataa kuyashika maagizo yangu na sheria zangu hata lini?

Kut. 16