44. lakini mtumishi wa mtu awaye yote aliyenunuliwa kwa fedha, ukiisha kumtahiri, ndipo hapo atamla pasaka.
45. Akaaye kwenu hali ya ugeni, na mtumishi aliyeajiriwa, wasimle pasaka.
46. Na aliwe ndani ya nyumba moja; usiichukue nje ya nyumba nyama yake yo yote; wala msivunje mfupa wake uwao wote.
47. Na wafanye jambo hili mkutano wa Israeli wote.