1. Basi majina ya wana wa Israeli walioingia Misri ni haya; kila mtu pamoja na jamaa zake walikuja pamoja na Yakobo.
2. Reubeni, na Simeoni na Lawi, na Yuda;
3. na Isakari, na Zabuloni, na Benyamini;
4. na Dani, na Naftali, na Gadi, na Asheri.
5. Na nafsi zile zote zilizotoka viunoni mwa Yakobo zilikuwa ni nafsi sabini; na huyo Yusufu alikuwa huko ndani ya Misri tangu hapo.