Kum. 6:12-16 Swahili Union Version (SUV)

12. ndipo ujitunze, usije ukamsahau BWANA aliyekutoa nchi ya Misri, nyumba ya utumwa.

13. Mche BWANA, Mungu wako; ndiye utakayemtumikia, na kuapa kwa jina lake.

14. Msifuate miungu mingine katika miungu ya mataifa wawazungukao;

15. kwani BWANA, Mungu wako, aliye katikati yako ni Mungu mwenye wivu; isije ikawaka juu yako hasira ya BWANA, Mungu wako, akakuangamiza kutoka juu ya uso wa nchi.

16. Msimjaribu BWANA, Mungu wenu, kama mlivyomjaribu huko Masa.

Kum. 6