12. ndipo ujitunze, usije ukamsahau BWANA aliyekutoa nchi ya Misri, nyumba ya utumwa.
13. Mche BWANA, Mungu wako; ndiye utakayemtumikia, na kuapa kwa jina lake.
14. Msifuate miungu mingine katika miungu ya mataifa wawazungukao;
15. kwani BWANA, Mungu wako, aliye katikati yako ni Mungu mwenye wivu; isije ikawaka juu yako hasira ya BWANA, Mungu wako, akakuangamiza kutoka juu ya uso wa nchi.
16. Msimjaribu BWANA, Mungu wenu, kama mlivyomjaribu huko Masa.