Kum. 5:3-13 Swahili Union Version (SUV)

3. BWANA hakufanya agano hili na baba zetu, bali na sisi, yaani, sisi sote tuliopo hapa, tu hai.

4. BWANA alisema nanyi uso kwa uso mlimani, toka kati ya moto;

5. (nami wakati ule nalisimama kati ya BWANA na ninyi, ili kuwaonyesha neno la BWANA; maana, mliogopa kwa sababu ya ule moto, wala hamkupanda mlimani); naye akasema,

6. Mimi ni BWANA, Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa.

7. Usiwe na miungu mingine ila mimi.

8. Usijifanyie sanamu ya kuchonga, mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, au kilicho chini duniani, au kilicho majini chini ya nchi.

9. Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi BWANA, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu, nawapatiliza wana uovu wa baba zao; hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,

10. nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu.

11. Usilitaje bure Jina la BWANA, Mungu wako; maana BWANA hatamhesabia kuwa hana hatia, mtu alitajaye jina lake bure.

12. Ishike siku ya Sabato uitakase, kama BWANA, Mungu wako, alivyokuamuru.

13. Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote;

Kum. 5