1. Musa akawaita Israeli wote, akawaambia, Enyi Israeli, zisikieni amri na hukumu ninenazo masikioni mwenu leo, mpate kujifunza na kuangalia kuzitenda.
2. BWANA, Mungu wetu, alifanya agano nasi katika Horebu.
3. BWANA hakufanya agano hili na baba zetu, bali na sisi, yaani, sisi sote tuliopo hapa, tu hai.
4. BWANA alisema nanyi uso kwa uso mlimani, toka kati ya moto;