21. Akajichagulia sehemu ya kwanza,Kwani ndiko lilikowekwa fungu la mtoa-sheria;Akaja pamoja na wakuu wa watu,Akaitekeleza haki ya BWANA,Na hukumu zake kwa Israeli.
22. Na Dani akamnena,Dani ni mwana-simba,Arukaye kutoka Bashani.
23. Na Naftali akamnena,Ee Naftali, uliyeshiba fadhili,Uliyejawa na baraka ya BWANA;Umiliki magharibi na kusini.
24. Na Asheri akamnena,Na abarikiwe Asheri kwa watoto;Na akubaliwe katika nduguze,Na achovye mguu wake katika mafuta.
25. Makomeo yako yatakuwa ya chuma na shaba;Na kadiri ya siku zako ndivyo zitakavyokuwa nguvu zako.