18. Na alaaniwe ampotezaye kipofu akakosa njia. Na watu wote waseme, Amina.
19. Na alaaniwe apotoaye hukumu ya mgeni, na yatima, na mjane aliyefiliwa na mumewe. Na watu wote waseme, Amina.
20. Na alaaniwe alalaye na mke wa baba yake, kwa kuwa amefunua mavazi ya babaye. Na watu wote waseme, Amina.
21. Na alaaniwe alalaye na mnyama wa aina yo yote. Na watu wote waseme, Amina.
22. Na alaaniwe alalaye na umbu lake, binti ya babaye, au binti ya mamaye. Na watu wote waseme, Amina.
23. Na alaaniwe alalaye na mkwewe, mamaye mkewe. Na watu wote waseme, Amina.
24. Na alaaniwe ampigaye mwenzake kwa siri. Na watu wote waseme Amina.
25. Na alaaniwe atwaaye ujira wa kumwua asiye makosa. Na watu wote waseme, Amina.