Kum. 23:9-13 Swahili Union Version (SUV)

9. Utakapotoka kwenda juu ya adui zako nawe u katika marago, jilinde na kila neno baya.

10. Akiwa kwenu mtu awaye yote asiyekuwa ni tohara kwa ajili ya yaliyomtukia usiku, na atoke nje ya kituo, wala asiingie ndani ya kituo;

11. lakini na iwe ikaribiapo jioni, yeye ataoga maji; na jua likiisha kuchwa ataingia ndani ya kituo.

12. Tena uwe na mahali nje ya kituo, kwa kutokea nje;

13. nawe uwe na jembe dogo katika silaha zako; napo uotamapo nje uchimbe kwa lile jembe, na kugeuka na kukifunika kikutokacho;

Kum. 23