6. Usitafute amani yao wala heri yao siku zako zote, milele.
7. Usimchukie Mwedomi; kwa kuwa ni ndugu yako; usimchukie Mmisri, kwa kuwa ulikuwa mgeni katika nchi yake.
8. Wana wao watakaozaliwa kizazi cha tatu na waingie katika mkutano wa BWANA.
9. Utakapotoka kwenda juu ya adui zako nawe u katika marago, jilinde na kila neno baya.
10. Akiwa kwenu mtu awaye yote asiyekuwa ni tohara kwa ajili ya yaliyomtukia usiku, na atoke nje ya kituo, wala asiingie ndani ya kituo;