Kum. 22:8-20 Swahili Union Version (SUV)

8. Utakapojenga nyumba mpya, fanya ukuta kando-kando ya dari lako, usije ukaleta damu juu ya nyumba yako, mtu akianguka huko.

9. Usipande shamba lako la mizabibu aina mbili za mbegu; yasije yakaondolewa matunda yote, mbegu ulizopanda na maongeo ya mizabibu yako.

10. Usilime kwa ng’ombe na punda wakikokota jembe pamoja.

11. Usivae nguo iliyochanganyikana sufu na kitani pamoja.

12. Ujifanyizie vishada katika pembe nne za mavazi yako ya kujifunika.

13. Mtu akitwaa mke, akamwingilia na kumchukia,

14. kisha akamshitaki mambo ya aibu kumzushia jina baya, akasema, Nimemtwaa mwanamke huyu, nami nilipomkaribia sikuona kwake alama za ubikira;

15. ndipo babaye yule kijana na mamaye watakapotwaa alama za yule kijana za ubikira, wawatolee wazee wa mji langoni;

16. na baba yake yule kijana awaambie wazee, Mwanamume huyu nilimpa binti yangu awe mkewe, naye amchukia;

17. angalieni, amemwekea mambo ya aibu, asema, Sikuona kwa binti yako alama za ubikira, nazo hizi ndizo alama za binti yangu za ubikira. Na wayakunjue yale mavazi mbele ya wazee wa mji.

18. Basi wazee wa mji ule na wamtwae yule mtu mume na kumrudi,

19. wamtoze shekeli mia za fedha, wampe babaye yule kijana, kwa kuwa amemzulia jina baya mwanamwali wa Israeli; naye awe mkewe; hana ruhusa ya kumwacha siku zake zote.

20. Lakini likiwa ni kweli neno hili, la kutoonekana kwake yule kijana alama za ubikira;

Kum. 22