Kum. 15:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Kila miaka saba, mwisho wake, fanya maachilio.

2. Na jinsi ya maachilio ni hii, kila mkopeshaji na akiache alichomkopesha mwenziwe, wala asimlipize mwenziwe wala nduguye; kwa kuwa imepigwa mbiu ya maachilio ya BWANA.

3. Waweza kumtoza mgeni; lakini kila uwiacho kwa nduguyo mkono wako utamwachilia.

4. Lakini hawatakuwako maskini kwenu; (kwa kuwa BWANA atakubarikia kweli katika nchi akupayo BWANA, Mungu wako, uimiliki, iwe urithi wako;)

5. kwamba utaisikiza tu kwa bidii sauti ya BWANA, Mungu wako, uyatunze maagizo haya yote nikuagizayo leo, kuyafanya.

Kum. 15