1. Kila miaka saba, mwisho wake, fanya maachilio.
2. Na jinsi ya maachilio ni hii, kila mkopeshaji na akiache alichomkopesha mwenziwe, wala asimlipize mwenziwe wala nduguye; kwa kuwa imepigwa mbiu ya maachilio ya BWANA.
3. Waweza kumtoza mgeni; lakini kila uwiacho kwa nduguyo mkono wako utamwachilia.