Kum. 14:8-19 Swahili Union Version (SUV)

8. na nguruwe, kwa kuwa amepasuliwa ukwato lakini hacheui, huyu ni najisi kwenu msile nyama zao, wala mizoga yao msiiguse.

9. Mtakula hawa katika wote walio majini; kila kilicho na mapezi na magamba mtakula;

10. na kila kisichokuwa na mapezi na magamba msile; ni najisi kwenu.

11. Mna ruhusa kula katika nyuni wote walio safi.

12. Lakini hawa msiwale; tai, na furukombe, na kipungu;

13. na kengewa, na kozi, na mwewe kwa aina zake;

14. na kila kunguru kwa aina zake;

15. na mbuni, na kirukanjia, na dudumizi, na kipanga kwa aina zake;

16. na bundi, na mumbi, na bundi mkubwa;

17. na mwari, na nderi, na mnandi;

18. na membe, na koikoi, kwa aina zake; na hudihudi, na popo.

19. Na wadudu wote watambaao wenye mabawa ni najisi kwenu; msiwale.

Kum. 14