14. na kila kunguru kwa aina zake;
15. na mbuni, na kirukanjia, na dudumizi, na kipanga kwa aina zake;
16. na bundi, na mumbi, na bundi mkubwa;
17. na mwari, na nderi, na mnandi;
18. na membe, na koikoi, kwa aina zake; na hudihudi, na popo.
19. Na wadudu wote watambaao wenye mabawa ni najisi kwenu; msiwale.
20. Mna ruhusa kula katika nyuni wote walio safi.