1. Ninyi akina bwana, wapeni watumwa wenu yaliyo haki na ya adili, mkijua ya kuwa ninyi nanyi mna Bwana mbinguni.
2. Dumuni sana katika kuomba, mkikesha katika kuomba huku na shukrani;
3. mkituombea na sisi pia, kwamba Mungu atufungulie mlango kwa lile neno lake, tuinene siri ya Kristo, ambayo kwa ajili yake nimefungwa,
4. ili niidhihirishe, kama inipasavyo kunena.
5. Enendeni kwa hekima mbele yao walio nje, mkiukomboa wakati.