Isa. 9:8-12 Swahili Union Version (SUV)

8. Bwana alimpelekea Yakobo neno, likamfikilia Israeli.

9. Nao watu wote watajua, yaani, Efraimu na yeye akaaye Samaria, wasemao kwa kiburi na kwa kujisifu nafsi zao,

10. Matofali yameanguka, lakini sisi tutajenga kwa mawe yaliyochongwa; mikuyu imekatwa lakini sisi tutaweka mierezi badala yake.

11. Kwa sababu hiyo BWANA atawainua adui wa Resini juu yake, naye atawachochea adui zake;

12. Waashuri upande wa mbele, na Wafilisti upande wa nyuma, nao watamla Israeli kwa kinywa kilicho wazi. Pamoja na hayo yote hasira yake haikugeukia mbali, lakini mkono wake umenyoshwa hata sasa.

Isa. 9