Isa. 7:11-15 Swahili Union Version (SUV)

11. Jitakie ishara ya BWANA, Mungu wako; itake katika mahali palipo chini sana, au katika mahali palipo juu sana.

12. Lakini Ahazi akasema, Sitaitaka, wala sitamjaribu BWANA.

13. Naye akasema, Sikilizeni sasa, enyi nyumba ya Daudi; Je! Ni neno dogo kwenu kuwachosha wanadamu, hata mkataka kumchosha Mungu wangu pia?

14. Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara. Tazama, bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamwita jina lake Imanueli.

15. Siagi na asali atakula, wakati ajuapo kuyakataa mabaya na kuyachagua mema.

Isa. 7