5. Lisikilizeni neno la BWANA, ninyi mtetemekao kwa sababu ya neno lake; Ndugu zenu wawachukiao ninyi, waliowatupa kwa ajili ya jina langu, wamesema, Na atukuzwe BWANA, tupate kuiona furaha yenu; lakini watatahayarika.
6. Sauti ya fujo itokayo mjini!Sauti itokayo hekaluni!Sauti ya BWANA awalipaye adui zake adhabu!
7. Kabla hajaona utungu alizaa;Kabla maumivu yake hayajampata,Alizaa mtoto mwanamume.
8. Ni nani aliyesikia neno kama hili?Ni nani aliyeona mambo kama haya?Je! Nchi yaweza kuzaliwa siku moja?Taifa laweza kuzaliwa mara?Maana Sayuni, mara alipoona utungu,Alizaa watoto wake.
9. Je! Mimi nilete wana karibu na kuzaliwa, nisizalishe? Asema BWANA; mimi nizalishaye, je! Nilifunge tumbo? Asema Mungu wako.
10. Furahini pamoja na Yerusalemu, shangilieni kwa ajili yake, ninyi nyote mmpendao; furahini pamoja naye kwa furaha, ninyi nyote mliao kwa ajili yake;
11. mpate kunyonya, na kushibishwa kwa maziwa ya faraja zake, mpate kukama, na kufurahiwa kwa wingi wa utukufu wake.