5. Tazama, utaita taifa usilolijua, na taifa lisilokujua wewe litakukimbilia, kwa sababu ya BWANA, Mungu wako, na kwa ajili yake Mtakatifu wa Israeli; maana amekutukuza.
6. Mtafuteni BWANA, maadamu anapatikana,Mwiteni, maadamu yu karibu;
7. Mtu mbaya na aache njia yake,Na mtu asiye haki aache mawazo yake;Na amrudie BWANA,Naye atamrehemu;Na arejee kwa Mungu wetu,Naye atamsamehe kabisa.
8. Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu; asema BWANA.