Isa. 5:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Na nimwimbie mpenzi wangu wimbo wa mpenzi wangu katika habari za shamba lake la mizabibu.Mpenzi wangu alikuwa na shamba la mizabibu,Kilimani penye kuzaa sana;

2. Akafanya handaki kulizunguka pande zote,Akatoa mawe yake,Akapanda ndani yake mzabibu ulio mzuri,Akajenga mnara katikati yake,Akachimba shinikizo ndani yake;Akatumaini ya kuwa utazaa zabibu,Nao ukazaa zabibu-mwitu.

3. Na sasa, enyi wenyeji wa Yerusalemu, nanyi watu wa Yuda, amueni, nawasihi, kati ya mimi na shamba langu la mizabibu.

4. Je! Ni kazi gani iliyoweza kutendeka ndani ya shamba langu la mizabibu nisiyoitenda? Basi, nilipotumaini ya kuwa litazaa zabibu, mbona lilizaa zabibu-mwitu?

Isa. 5