20. Haya, tokeni katika Babeli,Kimbieni kutoka kwa Wakaldayo;Hubirini kwa sauti ya kuimba, tangazeni haya,Yatamkeni mpaka mwisho wa dunia, semeni,BWANA amemkomboa mtumishi wake, Yakobo.
21. Wala hawakuona kiu alipowaongoza jangwani;Alitoa maji katika mwamba kwa ajili yao;Pia akaupasua mwamba, maji yakatoka kwa nguvu.
22. Hapana amani kwa wabaya, asema BWANA.