Isa. 48:19-22 Swahili Union Version (SUV)

19. Tena wazao wako wangalikuwa kama mchanga, na hao waliotoka katika tumbo lako kama chembe zake; jina lake lisingalikatika, wala kufutwa mbele zangu.

20. Haya, tokeni katika Babeli,Kimbieni kutoka kwa Wakaldayo;Hubirini kwa sauti ya kuimba, tangazeni haya,Yatamkeni mpaka mwisho wa dunia, semeni,BWANA amemkomboa mtumishi wake, Yakobo.

21. Wala hawakuona kiu alipowaongoza jangwani;Alitoa maji katika mwamba kwa ajili yao;Pia akaupasua mwamba, maji yakatoka kwa nguvu.

22. Hapana amani kwa wabaya, asema BWANA.

Isa. 48