Isa. 47:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Haya, shuka, keti mavumbini,Ewe bikira, binti Babeli;Keti chini pasipo kiti cha enzi,Ewe binti wa Wakaldayo;Maana hutaitwa tena mwororo, mpenda anasa.

2. Twaa mawe ya kusagia, usage unga;Vua utaji wako, ondoa mavazi yako,Funua mguu wako, pita katika mito ya maji.

3. Uchi wako utafunuliwa,Naam, aibu yako itaonekana.Nitalipa kisasi; simkubali mtu ye yote.

4. Mkombozi wetu, BWANA wa majeshi ndilo jina lake,Mtakatifu wa Israeli.

Isa. 47