1. Haya, shuka, keti mavumbini,Ewe bikira, binti Babeli;Keti chini pasipo kiti cha enzi,Ewe binti wa Wakaldayo;Maana hutaitwa tena mwororo, mpenda anasa.
2. Twaa mawe ya kusagia, usage unga;Vua utaji wako, ondoa mavazi yako,Funua mguu wako, pita katika mito ya maji.
3. Uchi wako utafunuliwa,Naam, aibu yako itaonekana.Nitalipa kisasi; simkubali mtu ye yote.