Isa. 46:11-13 Swahili Union Version (SUV)

11. Nikiita ndege mkali kutoka mashariki, mtu wa shauri langu toka nchi iliyo mbali; naam, nimenena, nami nitatekeleza; nimekusudia, nami nitafanya.

12. Nisikilizeni, ninyi mlio na moyo mshupavu, mlio mbali na haki;

13. Mimi ninaleta karibu haki yangu, haitakuwa mbali, na wokovu wangu hautakawia; nami nitaweka wokovu katika Sayuni kwa ajili ya Israeli, utukufu wangu.

Isa. 46