10. Mwimbieni BWANA wimbo mpya,Na sifa zake tokea mwisho wa dunia;Ninyi mshukao baharini, na vyote vilivyomo,Na visiwa, nao wakaao humo.
11. Jangwa na miji yake na ipaze sauti zao,Vijiji vinavyokaliwa na Kedari;Na waimbe wenyeji wa Sela,Wapige kelele toka vilele vya milima.
12. Na wamtukuze BWANA,Na kutangaza sifa zake visiwani.
13. BWANA atatokea kama shujaa;Ataamsha wivu kama mtu wa vita;Atalia, naam, atapiga kelele;Atawatenda adui zake mambo makuu.
14. Siku nyingi nimenyamaza kimya; nimenyamaza, nikajizuia; sasa nitapiga kelele kama mwanamke aliye katika kuzaa; nitaugua na kutweta pamoja.