Isa. 30:3-7 Swahili Union Version (SUV)

3. Basi, nguvu za Farao zitakuwa aibu yenu, na kutumainia kivuli cha Misri kutakuwa kufadhaika kwenu.

4. Kwa maana wakuu wake wako Soani, na wajumbe wake wamefika Hanesi.

5. Wote watawaonea haya watu wasioweza kuwafaidia, wasio na msaada wala faida, bali ni aibu na sababu ya kushutumiwa.

6. Ufunuo juu ya hayawani wa Negebu.Katikati ya nchi ya taabu na dhiki,Ambayo hutoka huko simba jike na simba,Nyoka na joka la moto arukaye,Huchukua mali zao mabegani mwa punda wachanga,Na hazina zao juu ya nundu za ngamiaWaende kwa watu ambao hawatawafaa kitu.

7. Kwa maana Misri huwasaidia bure, bila faida;Kwa hiyo nimemwita, Rahabu aketiye kimya.

Isa. 30