Isa. 3:19-26 Swahili Union Version (SUV)

19. na pete za masikio, na vikuku, na taji zao;

20. na dusumali, na mafurungu, na vitambi, na vibweta vya marashi, na matalasimu;

21. na pete, na azama,

22. na mavazi ya sikukuu, na debwani; na shali, na vifuko;

23. na vioo vidogo, na kitani nzuri, na vilemba, na utaji.

24. Hata itakuwa ya kuwa badala ya manukato mazuri kutakuwa uvundo, na badala ya mishipi, kamba; na badala ya nywele zilizosukwa vizuri, upaa; na badala ya kisibau, mavazi ya kigunia; na kutiwa alama mwilini kwa moto badala ya uzuri.

25. Watu wako waume wataanguka kwa upanga, na mashujaa wako vitani.

26. Na malango yake yatalia na kuomboleza, naye atakuwa ukiwa, atakaa chini.

Isa. 3