Isa. 3:17-23 Swahili Union Version (SUV)

17. Basi, kwa hiyo, Bwana atawapiga binti za Sayuni kwa pele za utosini, na BWANA ataifunua aibu yao.

18. Siku hiyo BWANA atawaondolea uzuri wa njuga zao, na kaya zao;

19. na pete za masikio, na vikuku, na taji zao;

20. na dusumali, na mafurungu, na vitambi, na vibweta vya marashi, na matalasimu;

21. na pete, na azama,

22. na mavazi ya sikukuu, na debwani; na shali, na vifuko;

23. na vioo vidogo, na kitani nzuri, na vilemba, na utaji.

Isa. 3