17. Basi, kwa hiyo, Bwana atawapiga binti za Sayuni kwa pele za utosini, na BWANA ataifunua aibu yao.
18. Siku hiyo BWANA atawaondolea uzuri wa njuga zao, na kaya zao;
19. na pete za masikio, na vikuku, na taji zao;
20. na dusumali, na mafurungu, na vitambi, na vibweta vya marashi, na matalasimu;
21. na pete, na azama,
22. na mavazi ya sikukuu, na debwani; na shali, na vifuko;
23. na vioo vidogo, na kitani nzuri, na vilemba, na utaji.