Isa. 27:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Katika siku hiyo BWANA, kwa upanga wake ulio mkali, ulio mkubwa, ulio na nguvu, atamwadhibu lewiathani, nyoka yule mwepesi, na lewiathani, nyoka yule mwenye kuzonga-zonga; naye atamwua yule joka aliye baharini.

2. Katika siku hiyo; Shamba la mizabibu la mvinyo, liimbieni.

3. Mimi, BWANA, nalilinda,Nitalitia maji kila dakika,Asije mtu akaliharibu;Usiku na mchana nitalilinda.

4. Hasira sinayo ndani yangu;Kama mibigili na miiba ingekuwa mbele zangu,Ningepanga vita juu yake,Ningeiteketeza yote pamoja.

Isa. 27