Isa. 26:2-7 Swahili Union Version (SUV)

2. Wekeni wazi malango yake,Taifa lenye haki, lishikalo kweli, liingie.

3. Utamlinda yeye ambaye moyo wake umekutegemeaKatika amani kamilifu, kwa kuwa anakutumaini.

4. Mtumainini BWANA siku zoteMaana BWANA YEHOVA ni mwamba wa milele.

5. Kwa kuwa amewashusha wakaao juu,Mji ule ulioinuka, aushusha,Aushusha hata nchi, auleta hata mavumbini.

6. Mguu utaukanyaga chini,Naam, miguu yao walio maskini,Na hatua zao walio wahitaji.

7. Njia yake mwenye haki ni unyofu;Wewe uliye mnyofu wainyosha njia ya mwenye haki.

Isa. 26