Isa. 24:10-13 Swahili Union Version (SUV)

10. Mji wa machafuko umebomolewa; kila nyumba imefungwa, asipate kuingia mtu awaye yote.

11. Pana kilio katika njia kuu kwa sababu ya divai; furaha yote imetiwa giza, na changamko la nchi limetoweka.

12. Ndani ya mji umebaki ukiwa, na lango lake limepigwa kwa uharibifu.

13. Maana katikati ya dunia, katikati ya mataifa, itakuwa hivi; kama wakati utikiswapo mzeituni, kama wakati waokotapo zabibu baada ya mavuno yake.

Isa. 24