19. Nami nitakusukuma na kukutoa katika mahali pako, naye atakushusha utoke hapa usimamapo.
20. Na itakuwa katika siku ile nitamwita mtumishi wangu Eliakimu, mwana wa Hilkia;
21. nami nitamvika vazi lako, nitamtia nguvu kwa mshipi wako, nami nitamkabidhi yeye mamlaka yako; naye atakuwa baba kwa wenyeji wa Yerusalemu, na kwa nyumba ya Yuda.
22. Na ufunguo wa nyumba ya Daudi nitauweka begani mwake; yeye atafungua wala hapana atakayefunga; naye atafunga wala hapana atakayefungua.