17. Tazama, BWANA atakutupa kwa nguvu, kama mtu mwenye nguvu; naam, atakuzonga-zonga.
18. Hakika atakukunja na kukutupa kama mpira, mpaka nchi iliyo mbali; huko utakufa, na magari ya utukufu wako yatakuwa kuko huko, ewe uliye aibu ya nyumba ya bwana wako.
19. Nami nitakusukuma na kukutoa katika mahali pako, naye atakushusha utoke hapa usimamapo.
20. Na itakuwa katika siku ile nitamwita mtumishi wangu Eliakimu, mwana wa Hilkia;