1. Ufunuo juu ya bonde la maono.Sasa una nini, wewe,Hata umepanda pia juu ya dari za nyumba?
2. Ewe uliyejaa makelele,Mji wa ghasia, mji wenye furaha;Watu wako waliouawa hawakuuawa kwa upanga,Wala hawakufa vitani.
3. Wakuu wako wote wamekimbia pamoja,Wamefungwa wasiutumie upinde.Wote walioonekana wamefungwa pamoja,Wamekimbia mbali sana.