Isa. 22:1-3 Swahili Union Version (SUV)

1. Ufunuo juu ya bonde la maono.Sasa una nini, wewe,Hata umepanda pia juu ya dari za nyumba?

2. Ewe uliyejaa makelele,Mji wa ghasia, mji wenye furaha;Watu wako waliouawa hawakuuawa kwa upanga,Wala hawakufa vitani.

3. Wakuu wako wote wamekimbia pamoja,Wamefungwa wasiutumie upinde.Wote walioonekana wamefungwa pamoja,Wamekimbia mbali sana.

Isa. 22