Isa. 14:15-20 Swahili Union Version (SUV)

15. Lakini utashushwa mpaka kuzimu;Mpaka pande za mwisho za shimo.

16. Wao wakuonao watakukazia macho,Watakuangalia sana, wakisema,Je! Huyu ndiye aliyeitetemesha dunia,Huyu ndiye aliyetikisa falme;

17. Aliyeufanya ulimwengu ukiwa, akaipindua miji yake;Asiyewafungua wafungwa wake waende kwao?

18. Wafalme wote wa mataifa wamezikwa wote kwa heshima,Kila mmoja ndani ya nyumba yake mwenyewe;

19. Bali wewe umetupwa mbali na kaburi lako,Kama chipukizi lililochukiza kabisa;Kama vazi la wale waliouawa,Wale waliochomwa kwa upanga,Wale washukao mpaka misingi ya shimo;Kama mzoga uliokanyagwa chini ya miguu.

20. Hutaungamanishwa pamoja nao katika mazishi,Kwa maana umeiharibu nchi yako,Umewaua watu wako;Kizazi chao watendao uovu hakitatajwa milele.

Isa. 14