Hos. 2:21-23 Swahili Union Version (SUV)

21. Tena itakuwa siku hiyo, mimi nitaitika, asema BWANA; nitaziitikia mbingu, nazo zitaiitikia nchi;

22. nayo nchi itaiitikia nafaka na divai na mafuta; nayo yataiitikia Yezreeli.

23. Nami nitampanda katika nchi kwa ajili yangu mwenyewe; nami nitamrehemu yeye asiyepewa rehema; nami nitawaambia wale wasiokuwa watu wangu, Ninyi ndinyi watu wangu; nao watasema, Wewe ndiwe Mungu wangu.

Hos. 2