Hos. 13:5-9 Swahili Union Version (SUV)

5. Mimi nalikujua katika jangwa, katika nchi yenye kiu nyingi.

6. Kwa kadiri ya malisho yao, kwa kadiri iyo hiyo walishiba; walishiba na moyo wao ukatukuka; ndiyo sababu wamenisahau mimi.

7. Basi nimekuwa kama simba kwao; kama chui nitavizia njiani;

8. nitakutana nao kama dubu aliyenyang’anywa watoto wake; nami nitararua nyama ya mioyo yao; na huko nitawala kama simba; huyo mnyama mkali atawararua.

9. Haya ndiyo maangamizo yako, Ee Israeli, ya kuwa wewe u kinyume changu mimi, kinyume cha msaada wako.

Hos. 13