Hos. 13:11-13 Swahili Union Version (SUV)

11. Nimekupa mfalme katika hasira yangu, nikamwondoa katika ghadhabu yangu.

12. Uovu wa Efraimu umefungwa kwa kukazwa; dhambi yake imewekwa akiba.

13. Utungu wa mwanamke mwenye mimba utampata; yeye ni mwana asiye na akili; maana wakati umewadia, ambao haimpasi kukawia mahali wapenyapo watoto.

Hos. 13