3. Tumboni alimshika ndugu yake kisigino;Na alipokuwa mtu mzima alikuwa na uwezo kwa Mungu;
4. Naam, alikuwa na uwezo juu ya malaikaAkashinda; alilia, na kumsihi;Alimwona huko Betheli, naye akasema nasi huko;
5. Naam, BWANA, Mungu wa majeshi;BWANA ndilo kumbukumbu lake.
6. Basi, mrudie Mungu wako; shika fadhili na hukumu; ukamngojee Mungu wako daima.