Hos. 12:10-14 Swahili Union Version (SUV)

10. Tena nimenena na hao manabii, nami nimeongeza maono, na kwa utumishi wa manabii nimetumia mifano.

11. Je! Gileadi ni uovu? Wamekuwa ubatili tu; huko Gilgali hutoa dhabihu za ng’ombe; naam, madhabahu zao zimekuwa kama chungu katika matuta ya mashamba.

12. Na Yakobo alikimbia mpaka Padan-Aramu,Na Israeli alitumika apate mke;Ili apate mke alichunga kondoo.

13. Na kwa nabii BWANA alimtoa Israeli katika Misri,Na kwa mkono wa nabii alihifadhiwa.

14. Efraimu amenitia hasira kali sana; kwa sababu hiyo damu yake itaachwa juu yake, na Bwana wake atamrudishia lawama yake.

Hos. 12