Hes. 9:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Kisha BWANA akanena na Musa katika bara ya Sinai, mwezi wa kwanza wa mwaka wa pili baada ya kutoka kwao katika nchi ya Misri, akamwambia,

2. Tena, wana wa Israeli na washike sikukuu ya Pasaka kwa wakati wake ulioagizwa.

3. Siku ya kumi na nne ya mwezi huu, wakati wa jioni, mtaishika kwa wakati wake ulioagizwa; kwa amri zake zote, na kama hukumu zake zote zilivyo, ndivyo mtakavyoishika.

4. Kisha Musa akawaambia wana wa Israeli kwamba waishike sikukuu hiyo ya Pasaka;

Hes. 9