Hes. 7:76-80 Swahili Union Version (SUV)

76. na mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi;

77. tena kwa ajili ya dhabihu ya sadaka za amani, ng’ombe wawili waume, na kondoo waume watano, na mbuzi waume watano, na wana-kondoo watano waume wa mwaka wa kwanza; hayo ndiyo matoleo ya Pagieli mwana wa Okrani.

78. Na siku ya kumi na mbili Ahira mwana wa Enani, mkuu wa wana wa Naftali;

79. matoleo yake yalikuwa sahani moja ya fedha, uzani wake ni shekeli mia na thelathini, na bakuli moja ya fedha, uzani wake shekeli sabini, kwa shekeli ya mahali patakatifu; vyombo hivyo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, kuwa sadaka ya unga;

80. na kijiko kimoja cha dhahabu, uzani wake shekeli kumi, kilichojaa uvumba;

Hes. 7