Hes. 7:71-78 Swahili Union Version (SUV)

71. tena kwa ajili ya dhabihu ya sadaka za amani, ng’ombe wawili waume, na kondoo waume watano, na mbuzi waume watano, na wana-kondoo watano waume wa mwaka wa kwanza; hayo ndiyo matoleo ya Ahiezeri mwana wa Amishadai.

72. Na siku ya kumi na moja Pagieli mwana wa Okrani, mkuu wa wana wa Asheri;

73. matoleo yake yalikuwa sahani moja ya fedha, uzani wake ni shekeli mia na thelathini, na bakuli moja ya fedha, uzani wake shekeli sabini, kwa shekeli ya mahali patakatifu; vyombo hivyo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, kuwa sadaka ya unga;

74. na kijiko kimoja cha dhahabu, uzani wake shekeli kumi, kilichojaa uvumba;

75. na ng’ombe mmoja mume mchanga, na kondoo mume mmoja, na mwana-kondoo mume mmoja wa mwaka wa kwanza, kuwa sadaka ya kuteketezwa;

76. na mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi;

77. tena kwa ajili ya dhabihu ya sadaka za amani, ng’ombe wawili waume, na kondoo waume watano, na mbuzi waume watano, na wana-kondoo watano waume wa mwaka wa kwanza; hayo ndiyo matoleo ya Pagieli mwana wa Okrani.

78. Na siku ya kumi na mbili Ahira mwana wa Enani, mkuu wa wana wa Naftali;

Hes. 7