Hes. 31:51-54 Swahili Union Version (SUV)

51. Musa na Eleazari kuhani wakapokea kwao hiyo dhahabu, maana, vile vyombo vyote vilivyofanyizwa.

52. Na dhahabu yote ya sadaka ya kuinuliwa waliyosongeza kwa BWANA, ya maakida wa elfu elfu, na maakida wa mia mia, ilikuwa shekeli kumi na sita elfu na mia saba na hamsini.

53. (Kwa kuwa hao watu wa vita walikuwa wametwaa nyara, kila mtu nafsi yake.)

54. Basi Musa na Eleazari kuhani wakapokea hiyo dhahabu mikononi mwa hao maakida wa elfu elfu na wa mia mia, na kuileta ndani ya hema ya kukutania, ili iwe ukumbusho kwa ajili ya wana wa Israeli mbele za BWANA.

Hes. 31